STORY:MALI YA KAFARA SEHEMU YA-5 - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

December 22, 2017

STORY:MALI YA KAFARA SEHEMU YA-5

STORY:MALI YA KAFARA
SEHEMU YA-5
MWANDISHI: Amany Zabranco.
Mainfo93.com

Sehemu iliyopita iliishia pale ambapo walikuwa wakimsubiri yule sungura aive vizuri ili waweze kumla. Sasa songa nayo.

Wakati kila mmoja akimmezea mate yule sungura,ghafra akatokea nyoka mkubwa akawa anataka kuwadhuru, yule muendesha mtumbwi akachukua kipande cha kuni chenye moto akaanza kupambana na yule nyoka, akafanikiwa kumchoma moto, kisha wakakaaa tena kuuzunguka ule moto wakaanza kula ile nyama ya sungura. Shabibi akakumbuka kwenye begi lake dogo alilokuwa amebeba mgongoni kuna pakti ya chumvi.

Akaanza kupekua ndani ya begi, vitu vyote vilikuwa vimelowa,akatoa pakti ya chumvi iliyolowa maji kisha akaanza kuikausha kwenye moto, ilipokauka wote wakaanza kuitumia kwa kupakaaa kwenye nyama ya sungura.
Wakala hadi kila mmoja akashiba kabisa kwa kuwa sungura alikua amenona, usiku ukawa umezidi sana ikabidi shabibi ajisogeze pembeni kidogo ya wenzake akajiegesha kidogo ili apate usingizi.

Pale kwenye moto akawa amebaki meresia na yule mwendesha mtumbwi, meresia naye taratibu akanyanyuka na kwenda pale alipojilaza shabibi.
Meresia akalaza kichwa chake kifuani kwa shabibi, wote wawili wakawa kila mmoja akimtamani mwenzake, shabibi akawa akimpapasa meresia kwenye nywele huku meresia naye akimpapasa shabibi kifuani.

Yule mwendesha mtumbwi akawa anawaona kina shabibi, nayeye akawa anatamani lakini yuko peke yake ikabidi ajisogeze pembeni ili awaache huru. Shabibi na meresia wakazidi kuzama ndani ya dimbwi zito la mahaba, wakasahau kama vyuma vimekaza ndani ya hilo pori, wakawa wanapapasana kwa hisia nzito huku kila mmoja akijawa na mihemuko kama bata mwenye nyege.
Hali ikawa si hali, mambo si habaaaa, wakawa wamepagawa kabisaa shida zote wakasahau na taratibuuuuu wakaanza kuingia kwenye dimbwi la kipekeee, kila mmoja akawa anasikika akitoa miguno na sauti mithiri ya tetere aliyenasa mtegoni.

Yule muendesha mtumbwi yeye akawa amesimama tu akiangalia miti na kupigwa baridi kali, mvua ya manyunyu ikaanza, kina shabibi ndio wakazidi kukorea hata manyunyu wakawa hawayahisi.

Ule usiku ukapita na tayari asubuhi kukawa kumekucha, wakajiandaaa kwa ajiri ya kuanza kusogea eneo la mto ili kutafuta msaada wa mtumbwi mwingine wakuweza kuwapeleka kwenye kile kijiji.

Wakatembea kwa dakika kadhaa hatimaye wakaiona mitumbwi minne kwa mbari ikiwa inakaribia walipokuwa,wakasimama kuisubiri hadi ilipowafikia kisha yule muendesha mtumbwi akanyoosha mikono juu kuashiria kuwa wanahitaji msaada.

Mitumbwi yote ikapunguza mwendo, waliposogea karibu zaidi wakamfahamu yule mwendeshaji kwa kuwa alikuwa ni mwenzao, ikabidi wawasaidie kwa kuwapakiza ndani ya mtumbwi.

Wakaanza safari ya kelekea kwenye kile kijiji huku kila mmoja akiwa anasikiliza story ya kile kilichowatokea kina shabibi usiku ule, wasafiri wengine wakawa wanaogopa yasije kuwatokea kama yaliyowakuta wenzao usiku.

Safari ikazidi kupamba moto hadi wakafika kwenye hicho kijiji, shabibi akawa anashangaa kwa jinsi kile kijiji kilivyo cha kidzaini ya aina yake, ni kijiji ambacho kina vutia kwa jinsi mazingira yake yalivyopambwa kwa vitu vizuri vya kiasiri, pia miti na maua yamepangiliwa kila njia ya kijiji, hata mabinti wa hicho kijiji wakawa wanavutia kiasi kwamba shabibi akawa anatumia muda mwingi sana kuwatazama, meresia akawa hapendezwi kuona shabibi muda wote anawatolea jicho warembo hao wa kijijini.

Meresia akamuomba shabibi wakapumzike kwenye mgahawa mmoja ili wapate chakula kabla ya kwenda kwa mganga, wakafika hadi sehemu kuna mgahawa mmoja umeandikwa "MALI YA KAFARA' ikabidi wasogee ili kujua kuna nini hapo, wakawa wanashangaaa kwa jinsi mgahawa huo ulivyopambwa kwa dizaini ya aina yake, ukiwa unavutia kwa mazingira mazuri ya usafi, shabibi akamuambia meresia waingie humo.

Yule muendesha mtumbwi naye akaingia humo, wakakutana na mabinti warembo wakiwa wamevaria mavazi ya kiasiri huku chuchu zikiwa zimesimama saa saba kasoro dakika moja mchana, shabibi akazidi kupagawa akawa anatoa jicho kufurahia uzuri wa mabinti hao.

Meresia akazidi kujawa na wivu akawa anatamani watoke nje, lakini  shabibi na yule muendesha mtumbwi wakazidi kupendezwa na vyuma vikali vilivyokuwa vikipishana kuhudumia wateja. Mabinti watatu wakasogea hadi kwenye meza nzuri waliyokuwa wamekaa kina shabibi, wakawauliza ni aina gani ya chakula wanahitaji.
Yule mwendesha mtumbwi akauliza
"kuna ugali na mrenda?".

Binti mmoja akajibu
"Ndio kaka, upo wa kutosha na uyoga,nyanya chungu na hata vingine vyote".

Shabibi akabaki amemuangalia yule binti aliyekuwa anaongea, akawa anazimezea mate zile chuchu, akawa anatamani amchukue, yule binti naye akawa anamregezea macho shabibi.

Meresia akaona lile tukio chozi likaanza kumlengalenga,ikabidi yule binti aondoke pale kwenye meza huku akigeuka nyuma kumtizama shabibi kwa jicho la mahaba.

Wale mabinti wengine nao wakawaambia kina shabibi kuwa kwenye huo mgahawa kila kitu unakula bure kabisa hutoi hata senti moja.
Shabibi akaona sasa huo ndo muda muafaka wa kutumia meno yake thelathini na mbili, akaagiza kuku mzima aliyekaangwa.
Meresia yeye akawa hata hataki kuagiza kitu kwa kuwa alipoona wale mabinti wanamvutia mtu wake akawa anawachukia, shabibi akaawaambia na yeye wamretee kuku.

Muendesha mtumbwi aliposkia msosi ni kujisevia, yeye akaagiza ugali pamoja na mboga zote za majani zilizopo pale, kweli wale mabinti wakaenda jikoni kwa ajiri ya kwenda kuleta chakula.

Baada ya muda kidogo, sahani swafi zinazong'aa zikaja huku zikiwa zimesheheni vyakula na matunda mazuri mazuri, shabibi akamuona tena yule binti anakuja huku kabeba sahani ya njano iliyojaa ma apple, shabibi roho yake ikawa inasuuzika mithiri ya barafu inayoyeyuka taratibu.

Akawa anatamani meresia aende hata uwani ili asikie hata sauti ya yule binti, binti naye akawa kisha nasa kwa shabibi akasogea kisha akatenga ile sahani ya ma apple mezani, huku akimuangalia shabibi machoni kwa jicho la mahaba.
Meresia wivu ukamzidi akasimama aka...........(ITAENDELEA @MAINFO93.COM. CRAFTED IN LOVE WITH MR.ZABRANCO).

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();