ST0RY:MJUKUU WA MSUKULE PART(10) - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 16, 2017

ST0RY:MJUKUU WA MSUKULE PART(10)

STORY:MJUKUU WA MSUKULE.
PART{10}.
MWANDISHI:#Amani zabranco.
                     Karibu sana mdau ujipatie mast0ry kila siku tembelea www.mainfo93.blogspot.com

Saguda akasema “je huyo shija walifanikiwa kumkamata??”.
Nyamizi akajibu “hamna hawakumpata kwa kua kipindi wanaenda kumfuata aliwahi kupata habari akatoroka hapa kijijini”.

       Saguda akasema “ikawaje?”
        Nyamizi akajibu “ikabidi nitafute mwanaume mwingine wa kunioa,lakini kila niliekua nampata aliishia kunichezea na kuniacha,japokua uzuri wangu ulikua unawavutia wengi. Mwishowe nikaja kupata huyu mume wangu ambaye ninaye sasa , yeye alikua  ni kijana mpole sana pia alikua akijituma sana katika kilimo cha mazao ya biashara, hivyo moyo wangu ukavutiwa nikawa namfuata kumuelezea hisia zangu, lakini kwa kua tayari nilikua nimesha zaa mtoto ikawa ni vigumu kwake kunikubalia”.

      
    Nyamizi akaendelea kusimulia “Akawa ananikatalia huku akisema kua yeye hayupo tayari kuoa inabidi nitafute mwanaume mwingine, nikambembeleza lakini akakataa kabisa, ndipo nikampata tajiri mmoja ndio akawa ananisaidia  matumizi, kumbe alikua ni muathirika wa ukimwi. Mimi bila ya kujua hili wala lile nikajua nimepata mtu wa kunioa, akawa ananipa vitu vya gharama, siku moja akaniambia tukutane kwenye lodge ya “Honey moon lodge” nikakubali siku hiyo nikajiandaa vizuri , nikawa najipamba ili azidi kunipenda. Nikaanza safari hadi sehemu Fulani,mara simu ikaita nilipoangalia nikagundua kua ni Yule mwanaume, nikapokea kwa haraka”. Akaniuliza nimefika wapi nikamueleza akasema nimsubiri pale anakuja kunipitia, baada ya dakika kadhaa ikaja gari karibu yangu ikapaki akashuka Yule mwanaume nikamkimbilia na kutaka kumkumbatai lakini kwa mbali nikamuona huyu mume wangu wa sasa roho ikanisuta nikaacha kumkumbatia Yule mwanaume, huyu mume wangu akawa anapita nikaona nibora nimuache huyu tajiri nikamkimbilia huyu mume wangu nikafika mbele yake nikamshika mkono, Yule tajiri akawasha gari akaondoka kwa hasira. Nikapiga magoti chini na kumuomba huyu mume wangu anikubalie kwa kua nilimpenda sana kutokana na tabia yake. Kweli siku hiyo akanikubalia hadi akafikia hatua ya kunioa baada ya siku kadhaa.

      Saguda akasema “nini kikafuata?”.

       Nyamizi akasema “kwa kweli huyu mume wangu alinipenda na kunijari sana; alikua akinihudumia  mimi na mwanangu kila kitu japo hakua ni mwanae, lakini kumbe mimi nilikua tayari nisha ambukizwa virusi vya ukimwi na wanaume niliotembea nao hapo zamani, hali yangu ikazidi kua mbaya sana nikazidi kudhoofika, mume wangu nae nikawa tayari nimesha muambukiza bila mimi kujua, nilijisikia vibaya nikajua nimeua kiumbe kisichokua na hatiya kwa kua mume wangu alinipenda sana. Hadi leo naishi na virusi vya ukimwi mimi na mume wangu na tunatumia dozi”……….itaendelea zidi kuifatilia upate uhondo)
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();