STORY:MJUKUU WA MSUKULE (PART14) - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 22, 2017

STORY:MJUKUU WA MSUKULE (PART14)




STORY:MJUKUU WA MSUKULE.
PART{14}.
MWANDISHI:#Amani zabranco.
                     Karibu sana mdau ujipatie mast0ry kila siku tembelea www.mainfo93.blogspot.com

         

Mara bibi yake naye akavua nguo kichawi akawa uchi kisha akasema “mkuu Yule kijana ambaye atarithi mikoba yangu ndio huyu nimemleta”. Yule mkuu akacheka kwa sauti ya juu “hahahahahahahahahahaha....” kisha akasema “sasa utakua umetimiza masharti ya mizimu”.

        Mkuu akawaamrisha walinzi  wamsogeze  Yule kijana mbele yake ili  ampe kiapo cha kurithi kiti cha bibi yake, lakini saguda akakataa  mbele ya mkuu kuapa kua atarithi uchawi wa bibi yake. Yule mkuu akakasirika akasema “sasa tunakupa adhabu ili ujifunze”. Mkuu akawaambia walinzi wamchukue na kumpeleka chumba cha  ‘MISUKULE’.Walinzi wakamchukua saguda kwa ajiri ya kumpeleka chumba cha misukule.

     Walipomfikisha mule ndani saguda hakuamini macho yake kuwaona watu  aliokua akiwafahamu kua walisha fariki miaka mingi iliyopita kumbe walikua bado wanaishi katika himaya ya kuzimu, wale misukule walikua wakiishi katika hali ya mateso makubwa. Saguda akawa anaogopa kuwasogelea wale misukule kwa kua walikua wanatisha sana huku nywele na makucha yao yakiwa marefu sana pia nywele zao zilikua ni chafu sana. Wale misukule wakawa wanaongea kama mabubu kwa kua walikua wamekatwa ulimi kila mmoja.
Kwa upande wa nyumbani kwa mzee zagamba wanashangaa hadi mida ya saa saba mchana saguda bado hajaamka kutoka chumbani kwake. Ikabidi mzee zagamba aingie ili kumuamsha lakini mzee zagamba akajawa na hofu kwa kua hakusikia hata sauti ya kuhema, ikabidi amshike kifuani ili kuangalia mapigo ya moyo, bahati mbaya moyo ukawa haudundi. Chozi na sura ya huzuni ikamjaa mzee zagamba kwa kujua kua tayari mwanae kisha fariki.

    Taratibu  zagamba akajaribu kunyanyua mkono wa saguda lakini ukawa umekakamaa, akamfunika vizuri na kumfumba macho kisha akatoka  nje  ili akamueleze mkewe sarafia. Lakini alipomuambia tu kuhusu ule msiba ghafla sarafia akastuka na kuanguka chini akazimia. Mzee zagamba akaita majirani wa karibu wakaja kumsaidia kumchukua sarafia kwa ajiri ya kumpeleka hospitali

    Baada ya masaa kadhaa habari zikazagaa kijiji kizima...(ITAENDELEA, USIPITWE)
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();