RASMI HII HAPA TAARIFA YA JKT FORM SIX MUJIBU WA SHERIA 2017 - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 24, 2017

RASMI HII HAPA TAARIFA YA JKT FORM SIX MUJIBU WA SHERIA 2017

                            INGIA WWW.MAINFO93.BLOGSPOT.COM    


MAINFO93, tunayo list ya wote waliochaguliwa na makambi yao, tuma jina lako na shule uliomalizia kwenda 0757035284, au airtel 0688139483 utalipa shilling elfu moja kwa mpesa au airtel money unajibiwa sms yako fasta fasta changamkia chance majina yapo yote mainfo93




TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limechagua vijana waliohitimu Elimu ya Sekondari Kidato cha Sita kwa mwaka 2017, kutoka Shule zote za Tanzania Bara kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria.
 Sanjari na Uchanguzi huo, JKT limewapangia Makambi watakayokwenda kupatiwa mafunzo kwa muda wa miezi mitatu na wanatakiwa kuripoti Makambini kuanzia tarehe 25 – 30 Mei 2017.
 Vijana waliochanguliwa, wamepangiwa katika kambi za JKT Rwamkoma – Mara, JKT Msange – Tabora, JKT Ruvu – Pwani, JKT Makutopora – Dodoma, JKT Mafinga – Iringa, JKT Mlale – Ruvuma, JKT Mgambo na JKT Maramba – Tanga, JKT Makuyuni – Arusha, JKT Bulombora, JKT Kanembwa na JKT Mtabila – Kigoma.
 Aidha, wahitimu wenye ulemavu wa kuonekana kwa macho (physical disabilities) wanatakiwa kuripoti kambi ya JKT Ruvu iliyopo Mlandizi mkoani Pwani ambayo ina miundombinu ya kuhudumia watu wa jamii hiyo.

JKT linawataka vijana hao kuripoti wakiwa na vifaa vifuatavyo:
  1. Bukta ya rangi ya ‘Dark blue’ yenye mpira kiunoni (lastic), iliyo na mfuko mmoja nyuma, urefu unaoishia magotini, isiyo na zipu.
  1. Raba za michezo zenye rangi ya kijani au blue.
  1. Shuka mbili za kulalia zenye rangi ya blue bahari
  1. Soksi ndefu za rangi nyeusi.
  1. Nguo za kuzuia baridi kwa waliopangiwa mikoa yenye baridi.
  1. Track suit ya rangi ya kijani au blue.
  1. Nauli ya kwenda makambini na kurudi majumbani.

Mkuu wa JKT anawakaribisha Vijana wote waliochaguliwa ili waweze kujiunga na Vijana wenzao katika kujifunza Uzalendo, Umoja wa Kitaifa, Stadi za kazi, Stadi za maisha na Utayari wa kulijenga na kulitumikia Taifa letu.


                          WWW.MAINFO93.BLOGSPOT.COM
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();