STORY:MJUKUU WA MSUKULE PART-8 - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 14, 2017

STORY:MJUKUU WA MSUKULE PART-8

STORY:MJUKUU WA MSUKULE.
PART{8}.
MWANDISHI:#Amani zabranco.
                     Karibu sana mdau ujipatie mastery kila siku tembelea www.mainfo93.blogspot.com

Sehemu iliyopita iliishia pale saguda alipofika na zawadi kwa wazazi wake, sasa tiririka nayo.

Wote wawili wakawa ni wenye furaha huku wakipendezwa na zile zawadi toka kwa saguda. Sarafia akasema “mwanangu saguda,sasa inabidi uende pale kwa dada yako nyamizi ukamsalimie maana anaumwa sana siku hizi. Saguda akakubali kwenda kumsalimia dada yake ambae alikua kisha olewa pale kijijini. Alipofika alishangaa kumuona ‘nyamizi’akiwa kakonda sana akamsalimia “dada za siku nyingi?, nyamizi akajibu ‘mbaya sana mdogo wangu saguda’. Saguda akatikisa kichwa kama ishara ya kusikitishwa na hali ya dada yake kisha akasema “pole sana dada, mbona umedhoofika hivyo?”,nyamizi akajawa na sura ya huzuni huku chozi likimtiririka mithiri ya manyunyu ya mvua akajibu “mdogo wangu,haya maisha we yaache tu kama yalivyo!!!!”.Saguda akauliza “ni nini kimekusibu dada yangu?”.
 Nyamizi akajibu “yani ni story ndefu sana, kwani toka nifeli shule, nikawa sina pa kwenda na maisha yakawa na ushawishi toka kwa mabinti wenzangu ambao walikua wakiniambia kua ili nipate mambo mazuri inabidi nitumie mwili wangu”.
    Saguda akauliza “ikawaje dada??”,
     Nyamizi akajibu “kutokana na hali duni ya maisha pamoja na umasikini  zikanifanya nianze kuuza mwili wangu kwa wanaume ili wanipatie fedha ya kununua vitu vizuri , tamaa ikazidi kunijaa nikawa nabadili nguo na viatu vya bei kali kila bada ya wiki moja.  Kutokana na uzuri wangu wanaume wengi pamoja na vijana wa rika langu wakawa wananitaka kimapenzi, bila ya kujua ninachokifanya ni hatari kwa afya yangu na kizazi changu”.

      Saguda akaina misha kichwa chini akawa anakumbuka hadithi za mtunzi mahiri aitwaye Amani zabranco akawa anahisi anachoki hadithia dada yake ni kama vile anasoma kitabu cha zabranco kumbe ndo yashamtokea.

          Saguda akauliza “kipi tena ambacho ni hatari  dada nyamizi??”.
           Nyamizi akajibu “ unapokua unaruhusu kijiti kichome kidonda chako kinachowasha,utajisikia raha ya kuondolewa muwasho, lakini iwapo kijiti kitakua ni cha mti wa mwiba mkali, basi maumivu yatakayo kuja badae ni makali kuliko ile hamu ya kidonda kuwasha”.


             Saguda akasema “una maanisha nini dada nyamizi?”………{je nyamizi alijibu niniiiii???? Usikose part8 hapahapa mainfo93)
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();