HOT STORY: MJUKUU WA MSUKULE (PART 18) - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 31, 2017

HOT STORY: MJUKUU WA MSUKULE (PART 18)



                                                      STORY:MJUKUU WA MSUKULE
                                                            PART(18)
                                                       MWANDISHI: Amani Zabranco
                                                          Mainfo93.blogspot.c
                                                          fb page facebook.com/Mainfo93
                                                    




Mara ghafra akaingia bibi kizee mmoja kwenye kile chumba cha kukatia ulimi,huku akiwa amevaa nguo kubwa nyekukundu mithiri ya joho la spika wa bunge. Yule bibi akawaambia wale walinzi
‘’niachieni huyu nimshughurikie mimi mwenyewe’’, wale walinzi wakaondoka akabaki saguda na yule kikongwe, kisha yule bibi akamtoa saguda pale walipokuwa wamemlaza kwa ajiri ya kumkata ulimi.

Bibi kizee akaanza kumuuliza saguda kuwa ni kivipi amefika   kwenye hiyo ngome  ya gamboshi??. Saguda  akamsimulia  jinsi ilivyokuwa  kisha yule bibi akaanza kutikisa kichwa  kwa kumuonea huruma saguda,yule bibi akatokea kuguswa na mateso anayoyapata saguda,akamuahidi kua atamsaidia mbinu za kutoroka kutoka kwenye ile gamboshi, yule bibi akasema
 ‘’kuanzia leo wewe  jina lako ni mjukuu wa msukule  kwa kuwa hilo  jina lina nyota kari itakayokusaidia kupambana na wachawi hadi kutoroka’’. Yule bibi akazidi kumuahidi saguda kuwa atamlinda  ili asikatwe ulimi kama misukule wengine, kikongwe akamchukua saguda na kumpeleka kwenye jengo alilokuwa akiishi yeye pale gamboshi. Usiku ulipofika yule bibi akaanza kumsimulia saguda jinsi nguvu ya kishetani inavyotumiwa na watu wengi.

Yule bibi akaanza kusema kwa sauti nzito iliyokuwa  ikijirudia mara mbili mbili ‘’mjukuu wangu binadamu wengi wenye mapesa na umaarufu katika jamii wanategemea sana nguvu za miujiza ili kufanikisha mambo yao. Pia wafanya biashara Zaidi ya asilimia 85% wanatumia nguvu za giza  ili kuvutia wateja’’.
Yule kikongwe akaendelea kusema ‘ndio maana uchawi  hauwezi kushuka nguvu miaka mia nane’’. Saguda akavutiwa na maneno ya yule bibi kisha akauliza ‘je wewe  ulianzaje kufanya hii kazi mbaya kabisaa???. Yule bibi akamjibu  kua ‘’nilifundishwa uchawi na shangazi yangu miaka mingi iliyopita, lakini sipendi na wewe mjukuu wangu uingie  kwenye   hii kazi ya kumuasi mungu’’.

Yule bibi alipotaja neono  mungu, saguda akastuka akamuuliza ‘’je na wewe  bibi unaamini mungu???’’. Yule kikongwe akajibu ‘’napenda sana mtu anaye amini mungu, kwa kuwa hata mimi nilikuwa ni muimbaji wa kikundi cha kwaya kanisani, nampenda mtu anayeamini mungu kwa kua huweza kuleta Amani, upendo na umoja katika jamii, lakini wachawi huleta chuki,fitina, kuua watu wasio na hatia pia huwa ni kikwazo cha maendeleo katiaka  jamii’’.
Saguda akauliza…………………(ITAENDELAAAA!!!!)

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();