STORY:MJUKUU WA MSUKULE PART7 - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 13, 2017

STORY:MJUKUU WA MSUKULE PART7

STORY:MJUKUU WA MSUKULE.
PART{7}.
MWANDISHI:#Amani zabranco.


Mkuu wa mila akatoa amri kua wale wanakijiji watatu wapigwe viboko  mbele ya wanakijiji ili liwe funzo kwa yeyote atakayekiuka makubaliano ya mkutano. Wakati wakisubiri kisiki cha mpingo aletwe, adhabu ya viboko ikazidi kutolewa kwa wale wanawake watatu.

 Mara gari la aina ya ‘kenta’ likaonekana likija taratibu  pale kwenye mkutano likiwa limebeba mizigo ya bibi kisiki cha mpingo. Akawekwa chini mbele ya wanakijiji kisha mzee zagamba akamuambia kuwa inabidi atoweke haraka pale kijijini. Wanakijiji wakafurahi kusikia kauli hiyo, bibi kisiki cha mpingo akachukuliwa na walinzi akaingizwa kwenye gari kwa ajiri ya kusafirishwa. Baada ya miezi kadhaa kupita huku kisiki cha cha mpingo akiwa kisha ondoka pale kijijini, neema ya mvua ikaingia , wanakijiji wakalima mazao yao na kuvuna kwa wingi sana.
Siku moja mzee zagamba akiwa amekaa nje akifurahia hewa safi itokayo kwenye miti mizuri iliyokua kando ya nyumba yake,mara kwa mbari akamuona kijana karibia na nyumbani kwake. Alipokaribia kumbe alikua ni mwanae wa kiume aliyekua masomoni. Mzee zagamba kwa shauku akamuita mkewe ‘sarafia’ aje kumpokea kijana wao mpendwa. Sarafia alipotoka nje hakuamini macho yake kumuona mwanae kipenzi karudi nyumbani , kwa shauku akasema.
“Waaaaaaaawwww,karibu sana baba angu” huku wakikumbatiana kwa hisia za kufurahia kuonana tena. Sarafia akasema “mwanangu pole sana na masomo”. Kijana akajibu “ahsante ,mama tayari nishapoa”. Mzee zagamba akadakia ‘mwanangu, wewe ndio jembe letu,kwa kua unajituma sana sio kama wenzako kina choroko wao kazi yao kulima tu hapa kijijini”.


 Sarafia akamletea kiti mwanae ili akae kwa ajiri ya kusalimiana na baba yake. Maongezi yakaendelea huku kila mmoja akifurahia kumuona mwenzake kwa mara nyingine tena.Kijana Yule aliyekua akijulikana kwa jina la ‘saguda’ akatoa zawadi ya simu za mkononi moja akampa baba yake na nyingine akampa mama yake. Lakini mama akasema “mwanangu hii simu mbona ni kama kioo cha kujiangalia?”,saguda akatabasamu kisha akajibu “Aaaaahhh.....mama hiyo inaitwa smartphone au screen touch”. Mama akatabasamu akasema “inabidi tupeane cozi ya namna ya kuitumia kwa sababu mimi na baba yako hatujawahi kuona simu kama hizi!”. Mzee zagamba akadakia “mimi mbona dakika hii tayari nisha anza kuielewa, ona  hapa nagusa kidogo tu kwa kidole yanakuja matufe mengi mengi, sema ndo sijaelewa yana maaisha nini”. Mama akadakia kwa kusema “nahisi moja hapo litakua ni la ile wanaitaka facebook”…………..(itaendelea) usikose kutembelea mainfo93
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();