MAHAKAMA YAIDHINISHA USHINDI WA KENYATA KENYA - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

November 20, 2017

MAHAKAMA YAIDHINISHA USHINDI WA KENYATA KENYA

Muhtasari

  1. Mahakama ya Juu Kenya imeamua uchaguzi wa marudio wa urais uliofanyika tarehe 26 Oktoba, 2017 ulikuwa halali.
  2. Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi wa uchaguzi huo baada ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga kususia uchaguzi huo.
  3. Mahakama ya Juu ilikuwa imebatilisha uchaguzi wa kwanza uliokuwa umefanyika tarehe 8 Agosti ambapo Kenyatta alikuwa pia ametangazwa mshindi.

Habari za moja kwa moja

Maandamano ya ghasia yafanyika ngome za upinzani Kenya

Uamuzi wa mahakama ya juu wa kuidhinishwa kwa ushindi wa rais Uhuru Kenyatta katika uchaguzi wa Oktoba 26 umezua maandamano ya ghasia katika maeneo yanayodaiwa kuwa ngome za upinzani nchini Kenuya.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation wafuasi wa kiongozi wa muungano wa Nasa Raila Odinga waliandamana ili kuonyesha kutoridhishwa kwao na uamuzi huo.
Maandamano hayo yalibadilika na kuwa ya ghasia katika maeneo kadhaa ya Nyanza, nyumbani kwa Odinga , katika maeneo ya Kibira na Mathare mjini Nairobi.
Mjini Kisumu, gari moja la kibinafsi lilichomwa katika eneo la Kondele muda mfupi baada ya ghasia kuzuka katika mji huo wa ziwa Victoria kufuatia uamuzi huo wa mahakama.
kulingana na gazeti hilo vijana walifunga barabara zinazoelekea mjini Kisumu kwa kuchoma magurudumu ya gari na mawe.
Waliwazuia watu watatu waliokuwa katika gari hilo la kibinafsi , wakawapiga na kuwaibia kabla ya kuliharibu gari hilo na kulichoma.
Watatu hao walikimbilia katika kituo cha polisi cha kondele wakihofia maisha yao.
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();