JERO ITAPENDEZA ZAIDI” YA DK SHIKA ISIINGIE USAJILI DIRISHA DOGO - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

November 13, 2017

JERO ITAPENDEZA ZAIDI” YA DK SHIKA ISIINGIE USAJILI DIRISHA DOGO

KESHOKUTWA Jumatano dirisha dogo la usajili litafunguliwa na timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara baada ya mechi 9, zitakuwa na nafasi ya kujipanga upya na kurekebisha sehemu am­bazo zinahitaji kufanya hivyo.
Baada ya mechi 9, timu zitakuwa zimeona kulingana na zilipo. Nafasi zipi baada ya kukusanya kiasi kipi cha pointi na zenyewe zinajua ukusanyaji wake wa pointi ulipita katika njia zipi.
Wakati wa kufanya usajili wa maboresho ya kikosi, hakika unahitaji utulivu wa hali ya juu kwa ajili ya kuhakikisha safari iliyobaki inasomeka kwa mwendo sahihi baada ya ma­badiliko.
Kuangalia kikosi kilivyo, mabao ya kufunga na kufungwa yalikuwa mangapi. Ushindi na sare yanakuwa ni matokeo ya ujumlisho wa kilichofanyika hasa baada ya kuangalia ‘per­formance’ mfano, walinzi walicheza vipi, tatizo la kiungo na ushambulizi limekaaje.
Maana yake iko hivi, ili kupata majibu sahihi wakati wa dirisha dogo na dira ya nini cha kufanya. Benchi la ufundi linapaswa kupewa na­fasi kubwa zaidi ya kufanya uamuzi wa kipi cha kupunguza au kuongeza na isiwe viongozi wenye matakwa au kero zao ndiyo wageuke kuwa makocha.
Lengo hasa ni kutaka kuwakumbusha viongozi wa timu yoyote ile inayoshiriki Ligi Kuu Bara kwamba suala la dirisha dogo la usajili, zaidi linakuwa ni ‘mali’ ya benchi la ufundi kwa kuwa ndilo limeona kwa ukaribu zaidi kilichopungua na wana nafasi kubwa ya kujua mahitaji kwa maana ya kipi hasa kinachotakiwa kuongezwa.

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();