STORY: MJUKUU WA MSUKULE PART5 - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

May 11, 2017

STORY: MJUKUU WA MSUKULE PART5





STORY:MJUKUU WA MSUKULE.
SEHEMU YA{5}.
MWANDISHI:#Amani zabranco.
                     Karibu sana mdau ujipatie mastery kila siku tembelea mainfo93
                
Sehemu iliyopita iliishia pale mzee zagamba alipokua akihutubia mkutano wa wanakijiji kuwaabia kua watunze hakula ili kumudu janga lililowapata, sasa endelea kutiririka
     ;kwa kipindi hiki cha msiba. Pia natoa salamu za rambi rambi kwa kila aliyepoteza ndugu yake katika janga hili.

      Mzee zagamba akaendelea kusema “kwa kua , tatizo hili ni la kwetu sote nimeamua kusimama hapa mbele yenu leo hii, ili kutoa suruhisho la mzozo uliokua ukitusumbua kwa mda mrefu hapa kijijini. Wanakijiji wote wakaonekana kua na hamu ya kujua jambo analotaka kusema mzee zagamba.
Mzee zagamba akaendelea kusema,”leo natangaza rasmi kua, mtu aliyekua akitusumbua kwa mda mrefu, bibi kisiki cha mpingo kuanzia leo hatutaki aishi kwenye hiki kijiji, pia kuanzia hivi sasa bibi ‘kisiki cha mpingo’ atatengwa na jamii nzima na hakuna mtu yeyote kwenda nyumbani kwake au kuonekana akiongea nae. Kwa atakaeenda kinyume na tamko la wakuu wa kimila atapewa adhabu ya kutengwa na jamii kwa mda wa siku tatu ikiwa ni pamoja na faini ya ng’ombe mmoja pamoja na gunia tatu za mpunga”.

        Wanakijiji wengi wakaonekana kushangilia huku miruzi na shangwe zikizidi kushamiri kwenye mkutano ule. Lakini kwa pembeni kukaonekana kikundi  kidogo cha wazee wanawake  pamoja na baadhi ya kina mama vijana ambao  wanaonekana kutofurahishwa na kauli ya mzee ‘zagamba’. Huku wakionekana kunong’ona chini chini.
Mzee zagamba akahitimisha kwa kusema “sasa hivi ulinzi wa kijiji utakaa kikao ili kupanga taratibu za kumfukuza bibi ‘kisiki cha mpingo”. Napenda kuwahimiza watu wote mfuate niliyo tamka hapa”. Kisha mkuu wa mila akasimama ili kufunga mkutano na kuwaamuru wana kijiji watawanyike.

Watu wakawa wanaondoka huku minong’ono ya hapa na pale ikizidi kusikika, lakini kile kikundi kilichokua pembeni kikawa kinaondoka kwa simanzi kuashiria kutofurahiswa na tukio hilo.Kile kikundi kikaondoka hadi karibia na nyumba ya bibi ‘kisiki cha mpingo’, lakini wengine wakaogopa kwenda kumsalimia wakihofia lile tamko la kwenye mkutano. Lakini wakatokea watu watatu, wawili wakiwa ni wazee wa kike na mmoja ni mwanamke kijana wakasema wao hawapo tayari kumtenga mtu  wao wa karibu.

      Wakaenda hadi kwake  wale wengine wakaendelea na safari ya kwenda makwao. Wale watatu walipokaribia kwa bibi ‘kisiki cha mpingo’ akawakaribisha huku akicheka kisha akawauliza; “vipi mbona wengine wamepitiliza?”. Yule mmama mmoja akadakia kwa shauku “yaani kuna tatizo kubwa,tena kubwa”. Kisiki cha mpingo akajawa na hofu akauliza……………..USIKOSE SEHEMU YA 6 Hapahapa @mainfo93

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();