Selemani Matola Awa Kocha Rasmi Lipuli Fc - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

June 28, 2017

Selemani Matola Awa Kocha Rasmi Lipuli Fc

“Ni kazi ngumu kwa sababu Lipuli ni timu ndogo na ngeni kwenye ligi na msimu ujao unatabiriwa kuwa mgumu lakini nitajitahidi kwa kushirikiana na viongozi wa timu kuhakikisha tunafanya vizuri,” amesema Matola.

Kocha huyo ambaye pia aliwahi kuifundisha Geita Gold Mine ya Geita amesema kazi yake kubwa hivi sasa itakuwa ni kukiimarisha kikosi chake kwa kusajili wachezaji wenye uwezo mkubwa.

Amesema katika kikosi chake anahitaji kuwa na wachezaji wazoeafu wasiopungua watano ambao atawachanganya na chipukizi wengine walioipandisha timu ili kujenga mchanganyiko mzuri.

“Najua ligi itakuwa ngumu lakini kama tutafanikiwa kusajili vizuri sioni kikwazo hapo naamini tutakuwa na kikosi imara na tutafanya vizuri kwa kutoa upinzani kama ilivyokuwa timu ngeni zilivyofanya vizuri huko nyuma.

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();