BAYERN YAMPA TALAKA KOCHA CARO ANCEROTI - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

September 28, 2017

BAYERN YAMPA TALAKA KOCHA CARO ANCEROTI

Kocha wa Bayern Munich Carlo Ancelotti amefutwa kazi leo kufuatia mwanzo mgumu wa msimu wa 2017/18 yakiwemo matokeo ya jana usiku ambapo timu hiyo ilikubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa PSG.
Mkurugenzi mtendaji wa Bayern Munich Karl-Heinz Rumminigge alionekana kuchukizwa na matokeo ambapo alisema Bodi ya timu itakuwa na kikao na kocha Ancelotti mchana wa leo baada ya timu kurejea kutoka Paris Ufaransa.
Mchana huu Sky Sports imethibitisha kuwa baada ya kikao Bodi imefikia maamuzi ya kusitisha kibarua cha kocha huyo raia wa Italia.
Ancelotti mwenye miaka 58 ameitumikia Bayern kwa msimu mmoja wa 2016/17 baada ya kuchukua nafasi ya Pep Gaurdiola ambaye alijiunga na Manchester City. Muitaliano huyo ameiwezesha Bayern kutwaa ubingwa wa Bundesliga msimu uliopita. Bayern Munich yamtimua Carlo Ancelotti

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();