RWANDAMINA AONA SIO FRESH KUTOENDA MAHAKAMANI. AMFUTA MANJI - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

September 18, 2017

RWANDAMINA AONA SIO FRESH KUTOENDA MAHAKAMANI. AMFUTA MANJI

Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina amekwenda moja kwa moja hadi katika mahakama ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kuteta na bosi wake wa zamani, Yusuf Manji.
Lwandamina alikutana na Manji katika viwanja vya mahakama ya Kisutu akiwa ameongozana na wasaidizi wake kam Shadrack Nsajigwa akiwemo Kocha wa Makipa wa Yanga, Juma Pondamali 'Mensah' na Meneja wa Yanga, Hafidhi Saleh.
Manji alikuwa mahakamani hapo kutokana na Kesi inayomkabiri Manji kuhusiana na kutumia madawa ya kulevya imeshindwa kusikilizwa leo katika mahakama ya Kisutu na kusogezwa mbele hadi Septemba 25.
Suala la kushindwa kusikilizwa ,limetokana na Manji kuchelewa kufika mahakamani, lakini naye alimueleza hakimu kuwa aliambiwa hakimu yuko katika kikao.
Kutokana na hali hiyo, imesogezwa mbele hadi Septemba 25, Manji atakapotakiwa kuleta mashahidi wake.
Manji anatuhumiwa kutumia madawa ya kulevya, jambo ambalo amekuwa akilikanusha.

'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();