KOCHA MPYA SIMBA,AFUNGUKA - MAINFO93

Latest

Kuwa updated kwa kutembelea mainfo93, hapa utakutana na mastory toka kila kona ya ulimwengu wa dot com. Contact habarimtandaoni@gmail.com

Random posts

January 26, 2018

KOCHA MPYA SIMBA,AFUNGUKA



HATIMAYE lile suala la subira ya kocha mpya wa Simba sasa limepata jibu kwa kuwa Kocha Pierre Lechantre ameanza kazi yake rasmi juzi kukinoa kikosi chake baada ya kukamilisha kila kitu.

Lechantre raia wa Ufaransa, anasaidiwa na makocha wengine wawili ambao ni Masoud Djuma raia wa Burundi pamoja na Mohamed Habibi kutoka Tunisia ambaye amejiunga na Simba akiwa pamoja na Lechantre.
Kocha huyo Mfaransa alitaka kujiunga na Simba akiwa na mtu kama Habibi ambaye anajua nini ampe cha kufanya na amekuwa akifanya naye kazi katika sehemu mbalimbali. Uongozi wa Simba umekubali ombi lake lakini umebaki na Djuma ambaye ameonyesha ni kocha anayeiweza kazi yake.
Akifanya yake.
Kuanza kazi kwa Lechantre na wasaizidi wake, maana yake Simba imekamilisha jambo moja inawezekana kabisa ni wakati mwafaka kuhamia katika jambo jingine kwa ajili ya muendelezo wa sahihi kinachotakiwa.
Unapokuwa na jambo fulani linalokusumbua, kawaida ukifanikiwa lazima kuna jingine linakuja mbele. Simba hawawezi kuwa na shida ya kocha pekee. Badala yake kuna mengine ya maendeleo yanafuatia na lazima wayatekeleze.
Kwa kuwa kama uongozi wametekeleza hilo moja, kunakuwa na majukumu mengine wanaendelea nayo kama kumuunga kocha huyo mkono katika masuala kadhaa kama atataka vifaa husika, uwanja wa mazoezi, kambi nzuri na kadhalika.
Simba wasitegemee kuona matunda bora kutoka kwa Lechantre na wasaidizi wake wakati wao hawatakuwa na ushirikiano na kocha huyo au kupuuzia mambo ambayo ata­waambia anahitaji kwa muda fulani ambao atawaeleza.
Kumekuwa na tabia, kocha anaingia kwa mbwembwe na viongozi watamuona kama lulu. Wakimzoea, basi anakuwa wa kawaida na mambo yanakwenda kama zamani.
'; (function() { var dsq = document.createElement('script'); dsq.type = 'text/javascript'; dsq.async = true; dsq.src = '//' + disqus_shortname + '.disqus.com/embed.js'; (document.getElementsByTagName('head')[0] || document.getElementsByTagName('body')[0]).appendChild(dsq); })();